Kuna watu hujituma sana katika kutafuta maisha lakini katika juhudi zao hawaonekani wafanya kitu cha maana au wakifanikiwa yote hii husababishwa na kuto kuwa na mipango thabiti na mizuri inayo tekelezeka , Hivyo wamejikuta wakitumia nguvu nyingi kutafuta lakini wamekuwa hawajui wanatafuta nini. Hali hii hufananishwa na mtu anae enda safarini bila kujua ni mahali gani anapokwenda hivyo safari yake huwa haina mwisho na hujikuta kila njia aionayo mbele yake kuifuata pasi kujua ni wapi inampeleka. Ndio maana leo tumekuletea somo hili juu ya namna ya kupanga mipango inayotekelezeka ili katika kila juhudi zako zionyeshe ni nini unacho kipagania.
Hatua ya kwanza: Tengeneza picha kubwa juu ya kitu unachotaka kufanya kwenye maisha yako. Hapa namaanisha kuwa katika akili yako lazima uwe na ufahamu juu ya kitu unacho taka kukifanya au unachotaka kukiona kinafanyika maishani mwako,, picha ambayo itasimama kama ndio ndoto ya maisha yako. picha hii itabeba kusudi la maisha yako, katika vitu vingi tunavyoona duniani vikifanyika vilianza katika hatua hii. Muhimu ni kuwa picha hii lazima iwe kubwa kwaakili za kawaida.
Hatua ya pili: Ni kubadili picha kuwa lengo kuu au kubwa zaidi la maisha yako (destination). Katika hatua hii unaanza kubadilisha ndoto au maono yako kuwa mpango utakao tekelezeka na kuifanya kuwa uhalisia. hatua hii haitofautini sana na hatua ya kwanza ila hapa ni muhimu zaidi kwasababu ni mahali ambapo mawazo hugeuzwa kuwa uhalisia na kuonekana kwa kila mtu , katika hatua hii ndio hufanya ndoto (mawazo) ya watu wengi kuishi miaka mingi kwasababu hata wanapokufa kuna watu huwa wanakuja kuendeleza iwapo mtu huyo aliishia sehemu fulani.
Hatua ya tatu: Ni kuligawa lengo kuu katika vipengele, ukisha fahamu juu ya lengo kuu la maisha yako katika hatua ya pili ni muhimu sasa kuligawa lengo hilo katika vipengele vidogovidogo ambavyo vitalenga kufikia lengo kuu. Mfano lengo unaweza ukagawa katika miaka yaani baada ya miaka au mda fulani niwe nimetimiza kufanya jambo fulani ambalo litakuwa linaelekea kutimza lengo kuu. lazima ufahamu namna ya kuvipanga na namna ya kuvifanya ili kutimiza malengo yako. Panga mipango ya miaka mitano, kila mwaka, kila baada ya miezi sita hata mwezi mmoja kama inawezekana na hakikisha kila mpango unahusiana na mpango uliopita.
Baada ya kupanga malengo yako zingatia yafuatayo:
-Hakikisha malengo hayo umeyaandika tena sehemu unayoweza kuiona kula siku au unayoweza kuisoma kila siku unapolala na unapo amka, hii itakupa hamasa zaidi ya kuyatimiza.
-Weka malengo yenye uharisia na yanayoweza kutimilika. Lazima uweke malengo ambayo yako chini ya uwezo wako na yanaweza kutimilizika. pasi nakuwa hakuna kisicho wezekana lakini ni muhimu pia kuangalia aina ya lengo kama linawezekana katika level uliyopo.
-Weka vipaumbele katika malengo yako. Katika mipango uliyo weka nilazima ufahamu kuwa kunampango lazima umfuate mwenzake yaani moja liwe na kupaumbele zaidi kuzidi lingine. kwahiyo yapange katika mfumo huo.
-Hakikisha unaweka orodha ya ratiba ya mambo unayotakiwa kufanya kila siku ili kutimiza lengo lako la maisha.
-Weka muda maalumu wakutimiza lengo yako, kwa maaana kwamba uweze kufahamu kama umefanikisha au uemefeli kutimiza lengo lako.
-Usikate tamaa katika kuipigania mipango yako, changamoto ni nyingi sana utazo kutana nazo unapokuwa ukipambana kuhkikisha malengo yako yanatimia hivyo unaweza kushindwa mara kadhaa au mambo kuonekana magumu, Fahamu tu yakuwa hiyo hli ni yakawaida muhimu tu ni kuto kata tamaa na kuamini kuwa iko siku malengo yako yatatimia.
Usiache kutembelea blog yetu kwa mafunzo mbalimbali kila siku na kushare kwa watu wengine ili ujumbe huu uweze kufika mbali zaidi na kuwasaidia watu wengine. pia unaweza ku comment ilituweze kupata maoni yako. Ahsante sana
SOMA ZAIDI ...
Hatua ya kwanza: Tengeneza picha kubwa juu ya kitu unachotaka kufanya kwenye maisha yako. Hapa namaanisha kuwa katika akili yako lazima uwe na ufahamu juu ya kitu unacho taka kukifanya au unachotaka kukiona kinafanyika maishani mwako,, picha ambayo itasimama kama ndio ndoto ya maisha yako. picha hii itabeba kusudi la maisha yako, katika vitu vingi tunavyoona duniani vikifanyika vilianza katika hatua hii. Muhimu ni kuwa picha hii lazima iwe kubwa kwaakili za kawaida.
Hatua ya pili: Ni kubadili picha kuwa lengo kuu au kubwa zaidi la maisha yako (destination). Katika hatua hii unaanza kubadilisha ndoto au maono yako kuwa mpango utakao tekelezeka na kuifanya kuwa uhalisia. hatua hii haitofautini sana na hatua ya kwanza ila hapa ni muhimu zaidi kwasababu ni mahali ambapo mawazo hugeuzwa kuwa uhalisia na kuonekana kwa kila mtu , katika hatua hii ndio hufanya ndoto (mawazo) ya watu wengi kuishi miaka mingi kwasababu hata wanapokufa kuna watu huwa wanakuja kuendeleza iwapo mtu huyo aliishia sehemu fulani.
Hatua ya tatu: Ni kuligawa lengo kuu katika vipengele, ukisha fahamu juu ya lengo kuu la maisha yako katika hatua ya pili ni muhimu sasa kuligawa lengo hilo katika vipengele vidogovidogo ambavyo vitalenga kufikia lengo kuu. Mfano lengo unaweza ukagawa katika miaka yaani baada ya miaka au mda fulani niwe nimetimiza kufanya jambo fulani ambalo litakuwa linaelekea kutimza lengo kuu. lazima ufahamu namna ya kuvipanga na namna ya kuvifanya ili kutimiza malengo yako. Panga mipango ya miaka mitano, kila mwaka, kila baada ya miezi sita hata mwezi mmoja kama inawezekana na hakikisha kila mpango unahusiana na mpango uliopita.
Baada ya kupanga malengo yako zingatia yafuatayo:
-Hakikisha malengo hayo umeyaandika tena sehemu unayoweza kuiona kula siku au unayoweza kuisoma kila siku unapolala na unapo amka, hii itakupa hamasa zaidi ya kuyatimiza.
-Weka malengo yenye uharisia na yanayoweza kutimilika. Lazima uweke malengo ambayo yako chini ya uwezo wako na yanaweza kutimilizika. pasi nakuwa hakuna kisicho wezekana lakini ni muhimu pia kuangalia aina ya lengo kama linawezekana katika level uliyopo.
-Weka vipaumbele katika malengo yako. Katika mipango uliyo weka nilazima ufahamu kuwa kunampango lazima umfuate mwenzake yaani moja liwe na kupaumbele zaidi kuzidi lingine. kwahiyo yapange katika mfumo huo.
-Hakikisha unaweka orodha ya ratiba ya mambo unayotakiwa kufanya kila siku ili kutimiza lengo lako la maisha.
-Weka muda maalumu wakutimiza lengo yako, kwa maaana kwamba uweze kufahamu kama umefanikisha au uemefeli kutimiza lengo lako.
-Usikate tamaa katika kuipigania mipango yako, changamoto ni nyingi sana utazo kutana nazo unapokuwa ukipambana kuhkikisha malengo yako yanatimia hivyo unaweza kushindwa mara kadhaa au mambo kuonekana magumu, Fahamu tu yakuwa hiyo hli ni yakawaida muhimu tu ni kuto kata tamaa na kuamini kuwa iko siku malengo yako yatatimia.
Usiache kutembelea blog yetu kwa mafunzo mbalimbali kila siku na kushare kwa watu wengine ili ujumbe huu uweze kufika mbali zaidi na kuwasaidia watu wengine. pia unaweza ku comment ilituweze kupata maoni yako. Ahsante sana