skip to main |
skip to sidebar
NJIA NZURI YA KUWAADHIBU WANAOKUCHUKIA BILA SABABU NI MAFANIKIO ENDELEVU.
MANENO HAYA AMEYAONGEA KIJANA MTANZANIA MWENYE MAFANIKIO ALIYEPITIA CHANGAMOTO NYINGI KATIKA MAISHA NA NDIYE MWALIMU WETU WA KAMPUNI YETU YA EGY BUSINESS SOLUTION,
anza kujifunza polepole uatmuelewa sana
Nasema; njia nzuri ya kuwaadhibu wanaokuchukia si kugombana nao
Mtandaoni au kuwanunia au kukunjiana nao ngumi, la hasha, huo ni mtindo
wa kizamani sana kumwadhibu mtu anayekuchukia bila sababu, njia ya
kisasa ni ipi? KUFANIKIWA SANA NA KUENDELEA KUFANIKIWA KWA MUDA MREFU.
Kwa kipindi kirefu sana niligombana na watu walionichukia
bila sababu, tena wengi ni wale ambao hata wakiulizwa "hivi ni kwanini
unamchukia Shigongo?" Huwa hawana jibu zaidi ya kusema " hata mimi
sijui....ila nalichukia tu" kuna watu huwa wanadhani mimi siumii, naumia
sana kwa bunadamu mwingine, haters wamewahi kumitesa sana, baadhi yenu
mnajua.
Siku moja nilisoma kwenye kitabu kimoja cheusi kiitwacho
Biblia, juu ya mtu aitwaye Yesu, ambaye siku zote nimedai ni rolemodel
wangu (ingawa sina uhakika kama naweza kumfia mtu mwingine kama
alivyofanya yeye) na kugundua kuwa pamoja na kuwa mtu mwema kwa
wayahudi, walimchukia, kumtafutia ubaya na mwisho wakamuua!
Pamoja
na yoye hayo hakuwachukia watu hawa, wala kigombana na. Kwake nzima
nzuri ya kuwaonyesha alikuwa sahihi haikuwa kubishana wa kupigana nao,
bali ilikuwa ni KUFUFUKA KUTOKA KATIKA WAFU, FULL STOP. Alipolifanya
hilo, haters wake wote walibaki kimya mpaka leo hii hawana tena cha
kusema.
Ndugu yangu unayesoma hapa,
Hata kama wewe ni mwema
vipi, siku zote watakuwepo tu watu wanaokuchukia ambao wangetamani hata
kuona umekufa! HUU NI UKWELI, YESU ALIKUWA MWEMA LAKINI WALIMUUA IWEJE
WEWE? NI UJINGA KUISHI KATIKA MAISHA HAYA UKISEMA " MIMI MGU MWEMA
HAKUNA ANAYEWEZA KUNIDHURU"
Hivyo basi Usibisha na haters wala
wasikupotezee muda kuwafikiria saaaana, mwisho watakunyong'onyeza na
kukuvuta hadi walipo wao ili mlingane na akosekane wa kumsema mwingine,
KATAA, WEKEZA NGUVU ZAKO KWENYE NDOTO NA MALENGO YAKO ILI UENDELEEE
KUFANIKIWA KWA HIYO NDIO ADHABU NZURI KWA HATERS, ambao wengi
husumbuliwa na wivu.
Nayasema haya sababu nina furaha mno kwa
mafanikio aliyoyapata Mtanzania Idriss usiku wa jana, ni heshima kubwa
kwa taifa letu. Kama unavyojua tena Simba akiwa watu wengi hujipaka damu
yake ili waoonekana mashujaa, na mimi ni mmoja wao, nimefurahishwa sana
na ushindi wake na ingawa sikumpigia kampeni hapa facebook, sio vibaya
kumshangilia kwa ushindi wake ambao mwisho wa siku ni wa kila
Mtanzania.
Onyo langu tu kwake ni kwamba, awe makini sana na watu
watakaomzunguka kuanzia sasa, awe na uwezo wa kuchuja nani rafiki na
nani mpambe! Najua anayo mipango aliyokuwa nayo kabla ya ushindi pengine
aliwahi kusema " siku nikipata fedha nita..." Ni vizuri kuyatazama hayo
kabla kukurupukia mambo mengine, najua waalimu watakuwa wengi, malengo
yakiwa kutumbua.
Namhakikishia, wapo watakaojitolea kumbebea mkoba,
kumsifia, kumfungulia mlango wa gari, kumletea wasichana wazuri na
kadhalika, anachotakiwa kufanya ni kutulia, fedha na mafanikio ndivyo
yalivyo, asibabaike bali ajiamini na kuangalia ndoto zake na kutumia
fedha hizi kuzitimiza.
Mafaniko aliyoyapata ni adhabu tosha kwa
haters wake, lakini lazima aelewe kuwa adhabu nzuri kwa haters sio tu
mafanikio bali Mafanikio Endelevu. Haters ni kama Fungas wakioewa nafasi
huchipuka tena.
Yeye sio wa kwanza kushinda fedha hizi, wapo
walioshinda kabla yake, wapo wapi? Wanafanya nini? Au wameharibu na
kuwapa nafasi haters ya kuendelea kuwaumiza mioyo? Ajifunze kutoka kwa
hao na asirudie makosa yao, akumbuke milioni 500 si pesa nyingi tena
siku hizi kama iliyokuwa miaka michache iliyopita, akiendeleza starehe
na sifa za hapa mjini muda si mrefu akaunti itasoma 000000! Hapo ndipo
ataelew kumbe hata waliokuwa wamemzunguka pia walikuwa haters. Itakuwa "
yuko wapi ndugu yenu......sisi tulikuwa tunamwangalia tu....bado
anaishi kwa mama yake...."
Akumbuke adhabu nzuri kwa haters ni mafanikio makubwa na endelevu.
AMEN.
0 comments:
Post a Comment