.

.

MUNA TOYS & STATIONERY

MUNA TOYS & STATIONERY

Thursday, August 17, 2017

"MC ELIUD TROTAR" PROGRAMU YA MAZOEZI INAYOKUJA KWA KASI


Baada ya MC ELIUD SAMWEL kusaini mkataba na kujiunga na kampuni ya EGY BUSINESS SOLUTION siku kadhaa zilizo pita , Sasa ameamua kuja na programu ya mazoezi ya mwili iendayo kwa jina la MC ELUD TROTAR ambayo ilizundiliwa rasmi siku ya tarehe 12 -8-2017 ambayo ilikuwa nimaadhimisho ya siku ya vijana duniani, Programu hiyo itahusisha mazoezi ya mwili kama vile mbio za kawaida, mazoezi ya viungo na matembezi ya kawaida yote hii ni kwaajili ya kuuweka mwili salama. Mazoezi hayo yatakuwa yakifanyika kila siku ya jumamosi kuanzia saa kumi na mbili kamili asubuhi hadi saa mbili ambapo mbio za kawaida zitakuwa zikianzia eneo la njia panda Halengo au JKT CARWASH kuelekea uwanja wa mpira wa HALENGO uliopo karibu na kanisa la ROMAN KATOLIKI shughuli zote zitakuwa ziki malizikia mahali hapo.

MC ELIUD SAMWEL alielezea kuhusu programu hiyo yakuwa itakuwa niya mda mrefu na lengo kubwa ni kuwafanya vijana wa Mbeya kuwa na mazoea ya kufanya mazoezi ya miili yao mara kwa mara ili kujijenga kiafya. Lakini pia kuwaleta vijana wa Mbeya pamoja ili kufanya mambo mbalimbali yatakayo leta matokeo chanya kwenye jamii inayo tuzunguka. Nakusema kuwa anamipango mingi sana kupitia programu hii ambayo itafanyika siku zijazo pasipo kuizungumzia kiundani mipango hiyo.

Mwisho aliwashukuru sana watu wote walio muunga mkono katika siku hiyo ya kwanza kwa kujitokeza kufanya mazoezi hayo na kuanza rasmi kwa kampeni hiyo ya MC ELIUD TROTAR pia aliwashukuru uongozi wa kampuni ya EGY BUSINESS SOLUTION kwa kusimamia na kufanikisha shughuli hiyo. Zaidi alizidi kuwahimiza vijana kujitoa na kuunga mkono programu hiyo kwasababu ina manufaa kwa kila mmoja atakae shiriki katika kuujenga mwili  ili hali kila mmoja wetu anafahamu umuhimu wa mazoezi katika miili yetu.    Kwa maelezo zaidi kuhusu programu hiyo na ushiriki wake wasiliana nao kupitia namba 0689458877 au 0767187092 na kuona updates za matukio hayo tembelea kurasa za facebook @MC ELIUD SAMWEL na instgram @MC_ELIUDSAMWEL_EVENTS na kurasa zote za   EGY BUSINESS SOLUTION




            Hapa ndio JKT CARWASH mahali ambapo mazoezi huanzia kuelekea viwanja vya Halengo



                                  Viwanja vya Halengo mazoezi yalipo anza.














            Mc Eliud Samwel akitoa maelezo baada ya mazoezi

                      Baada ya mazoezi baadhi ya washiriki wakipata picha ya pamoja.

0 comments:

Post a Comment

 

Bongo Blogs - Blog ya Taifa

COPYRIGHT © Egy business solution DESIGN BY NANG JET 0764504595,0672804085