.

.

MUNA TOYS & STATIONERY

MUNA TOYS & STATIONERY

Tuesday, July 1, 2014

UKITUMIA HII FALSAFA YA WANAJESHI WA UGIRIKI KUCHOMA MELI MOTO, MAMBO MENGI MAISHANI UTAYASHINDA






Kuchoma meli moto (BURN THE BOAT)  ni falsafa ambayo ilikuwa ikitumiwa na jeshi  la wagiriki ANCIENT GREEK WARRIOS miaka ya nyuma  falsafa hii iliwajenga wanajeshi hawa kufanya bidii zote na hatimaye kushinda kila vita waliyokuwa wanapigana miaka hiyo

Wanajeshi hawa walipokuwa wanaenda  kupigana vita na nchi nyingine kutokana na zamani ilikuwa sio rahisi kwa  wao kutumia  ndege kwao njia iliyokuwa rahisi ni kutumia meli kwa kubebea wanajeshi pamoja na silaha zao, 

Walipofanikiwa kufika ng’ambo ya maadui zao yaani ng’ambo ya nchi nyingine, njia pekee kamanda wao wa  jeshi alichowaamuru ni  kuichoma meli yao ambayo iliwasaidia kufika ng’ambo na wao kubaki  na silaha pekee,  na kuanza mapambano na maadui zao,  

wao tukio hili kwao la kuchoma meli (BURN THE BOAT) lilikuwa na maana kubwa kwao kwani liliwajaza nguvu ya kuendelea kupambana kwani kurudi nyuma  au kufanya utegezi wa namna yoyote ile kwao kusingewasaidia kitu kwani usafiri ulio wawezesha wao kufika ng’ambo hiyo ulikuwa umeisha teketea kwa moto

Hivyo njia pekee iliyowabakia ni kupambana au kufa yaani (COMPETE OR DIE) kwani ilikuwa hamna  njia nyingine ya kusalimika kwao kwani meli ilikuwa haipo,hii iliwajenga katika vitu kadhaa ikiwa ni pamoja na kuwa
1.       HAKUNA KUKATA TAMAA (kwani hata ukikata tamaa usafiri wa kukurudisha nyumbani haupo)
2.       HAKUNA KURUDI NYUMA (meli haipo)
3.       HAKUNA KUJITETEA WALA KUJISALIMISHA KWA ADUI

    
 Wanajeshi waliposhuhudia meli zao zikichomwa moto akili zao zilichojaa ni kupambana mpaka washinde , kwani kulikuwa hamna njia mbadala

   KATIKA MAISHA YETU
Tumekuwa tukikutana na vikwazo vingi sana katika maisha yetu hivyo kutufanya kuto kusonga mbele aidha ya kuogopa kuchekwa na marafiki, ndugu na kukatishwa nao tamaa , na wengi wameshindwa kuendelea mbele katika maisha kwa sababu ya kuogopa kufanya maamuzi ya vitu wanavyo viamini katika ndoto zao,

Wengi wa marafiki zetu wamekuwa wakitusimulia mipango na ndoto walizonazo ila  imekuwa shida kwao kuanzisha na kuanza kuzitenda. Sasa njia sahihi kwako ni KUCHOMA MELI MOTO kwa jambo unalotaka kulianzisha yaani amua kulifanya kwani kurudi au kutazama nyuma hakuta kusaidia,

Vijana wengi tumekuwa na ndoto za kuanzisha vitu mbalimbali ila tumekuwa tukikumbwa na ugonjwa mkubwa ambao unaitwa FEAR(HOFU) ambayo njia sahihi ukitaka kufanikiwa katika ndoto zako ni wewe kuamua KUCHOMA MELI YAKO YA HOFU MOTO na kuiamini ndoto na malengo na amua leo kuanza na kuanzisha hilo jambo unaloliamini,

Unania ya kuingia katika ujasiriamali, biashara ya namna yoyote ni kipindi chako cha sasa kuamua KUCHOMA MELI MOTO nakuingia rasmi huku ukiamini ndoto zako na kamwe usitazame watu ambao wameshindwa au wanao kukatisha tamaa kikubwa ni kuto kataa na tumia falsafa ya WAGIRIKI 

kwao meli kuwepo pembeni ilikuwa ikiwatia uvivu, kwahiyo kwao njia bora ni kuzichoma meli moto

0 comments:

Post a Comment

 

Bongo Blogs - Blog ya Taifa

COPYRIGHT © Egy business solution DESIGN BY NANG JET 0764504595,0672804085