.

.

MUNA TOYS & STATIONERY

MUNA TOYS & STATIONERY

Tuesday, February 3, 2015

FANYA HIVI ILI UYAFURAHIE MAISHA YAKO 2015




Tumekuwa tukitafuta namna mbalimbali ambazo tunaweza kuyafanya maisha yakawa mazuri zaidi kuliko tuliyonayo kwa sasa, sisi kama EGY BUSINESS SOLUTION tunakuletea hizi sababu kwa uchache tuu namna ya wewe kuyafurahia maisha yako, kama ifuatavyo



WAPE WATU ZAIDI YA WANAVYOTEGEMEA 

Mara nyingi watu wanategemea kuwa uwezo wako utakomea kwenye eneo flani, huku wakijijengea uhakika wa asilimia zote kuwa siajabu utaishia pale, lakini jambo kubwa sana ambalo ukitaka kuyafurahia haya maisha ni wewe kufanya jambo zaidi hata ya wengine wanavyotegemea , BINADAMU WANAHAMU KUBWA SANA KUWA UISHIE PALE WANAPOPAONA WAO.  Usitishike hata kama wao wanasema mara kwa mara JIAMINI WEWE NA FANYA ZAIDI YA WANAVYOTEGEMEA

KAMA UNAMPENDA MTU BASI MAANISHA
namna yoyote ya kufikia furaha ya ndani mwako ni kujenga upendo kwa binadamu wanaokuzunguka na ikitokea unampenda mtu yeyoto hakikisha UNA MAANISHA, hata ukipata nafasi ya kumwambia unampenda hakikisha inatoka ndani kabisa

ACHA KUYAAMINI YOTE AMBAYO UNAYASIKIA
Mara nyingi katika ongea yetu tumekuwa tukisisitiza sana namna tunavyokutana na sauti nyingi sana humu duniani, hivyo na mpaka mwisho wa dunia tutasikia mengi, ila chunga sana  kuyaamini yote unayoyasikia, kila sauti inaweza kukuambia la kwake na zitakuja za kukutia moyo, kukatisha tamaa, USIAMINI KILA SAUTI UNAZOZISIKIA   

USICHEKE AU USIMCHEKE MTU YEYOTE KUHUSIANA NA NDOTO ZAKE
Kila binadamu anacho kitu ambacho anakiona ndani mwake na kiu ya mafanikio anayotaka kuifikia usijaribu kuanza kuicheka na kuidharau, haujui nguvu ambayo ameiweka kuifanikisha ndoto yake.kuna msemo huwa unasemwa USICHEKE JAMBO USILOLIJUA MWISHO WAKE

IKIWA UMEJUA KUWA UMEKOSEA, CHUKUA HATUA YA KUJIREKEBISHA
Hakuna binadamu ambaye hajawahi kufanya makosa kikubwa tulichotofautiana ni viwango na aina ya makosa tuliyoyafanya , sasa makosa kwako yaweke kama somo na amini kuwa upo dunia darasa hivyo kukosea ni jambo a kawaida sana. Kikubwa sana kwako ni hili hapa unapobaini kuwa umekosea basi ichukue hatua ya haraka KUREBISHA UTAFANIKIWA

MUDA MWINGINE JIPE MUDA WAKUKAA MWENYEWE, UJUE KITU CHA KUIPA DUNIA
kukaa muda mwingine peke  yako kunakupa furaha sana, kwani unakuwa na muda mzuri wa kuipa dunia na kujua ufanye nini kwa ajili ya watu wengine na wewe pia , hatimaye kuelekea mafanikio   yale uyatakayo katika uhai wako 

AHSANTENI KARIBUNI KUFANYA KAZI PAMOJA NA SISI KATIKA MAMBO MBALIMBALI





0 comments:

Post a Comment

 

Bongo Blogs - Blog ya Taifa

COPYRIGHT © Egy business solution DESIGN BY NANG JET 0764504595,0672804085