.

.

MUNA TOYS & STATIONERY

MUNA TOYS & STATIONERY

Wednesday, June 18, 2014

TEAM CHALLENGE, SAFARI YA VIJANA WA KITANZANIA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO.KWA LENGO LA KUPAZA SAUTI ZAO ZISIKIKE



   TEAM CHALLENGE, SAFARI YA VIJANA WA KITANZANIA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO.KWA LENGO LA KUPAZA SAUTI ZAO ZISIKIKE


YMCA world Alliance yenye makao mkuu Geneva, Switzerland pamoja na baraza la vijana la YMCA Tanzania lenye makao yake makuu mjini moshi, chini ya uratibu wa kampuni la vijana wa kitanzania TANPICTURES UNIVERSAL waliandaa tukio kubwa kwa vijana nchini Tanzania waliandaa tukio na kushiriki wiki ya vijana iliyopewa jina la Y’s VOICE SUMMIT ndani ya siku saba kuanzia tarehe 02.06.2014 hadi 08.06.2014

 Ambayo  vijana wa kitanzania waliungana na vijana zaidi ya milioni 58 toka nchi zinazounda umoja  wa YMCA (world Allience). Jambo muhimu ni kuunga mkono kaulimbiu ya vijana itakayowezesha mabadiliko sahihi ya uundwaji sera za kimaendeleo kuanzia ngazi ya nchi hadi dunia. 

Hii ni pamoja na vijana watanzania kupata fursa ya kueleza mawazo, hisia na maoni yao katika mambo makuu yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na SERA UWEZESHWAJI, NAFASI YA KIJANA KATIKA UONGOZI NA MASUALA YAHUSUYO AFYA na AJIRA hasa suala la ajira binafsi kwa njia ya kipaji

Maadhimisho haya ya siku ya vijana dunia yalihusisha vijana kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania ikiwa ni pamoja na vijana kutoka MBEYA, TANGA, MOSHI,DAR ES SALAAM, ARUSHA, DODOMA,MANYARA, ambao kwa pamoja waliweza kufanikisha wiki ya vijana duniani  na
 Wadhamini wakuu wa safari hii ni kampuni bora la utalii ZARA(WWW.ZARATOURS.COM) lililopo mjini moshi, na AZAM na supermarket ya kisasa ya MARENGA

MADHUMUNI YA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO
1.kuwahamasisha vijana  watanzania na kupandisha bendera yenye ujumbe  wa mwaka 2014 kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro kwa ishara na alama ya kusikika
2.kutangaza utalii na utamaduni wetu kwani watu wengi watashuhudia hili likifanyika kwenye kilele hiki ambacho ni kivutio kwa wengi
   ‘NASIMAMA KWA AJILI YA VIJANA NA NINATAKA SAUTI YAO ISIKIKE’
                                       Team challeng vijana wakiwa YMCA TANZANIA

              vijana walipopata fursa ya kutembelea kampuni bora la utalii ZARA(www.zaratours.com) mjini moshi

TEAM CHALLENG kwa mwaka 2014 walipandia njia ya marangu hapa ndipo safari ilipo anzia wakiwa na kiu ya kufika kilele cha mlima mrefu barani africa
                                          njiani ilikuwa furaha tuu na nyimbo kwa pamoja

                              vijana TEAM CHALLENG wakiwa HOROMBO mita 3720 kutoka usawa wa bahari
 ZEBRA ROCKS ni eneo la kuvutia sana lenye hali ya ubaridi na rahisi kukiona kilele cha mawenzi kwa urahisi

                                     GILMAN'S point eneo la juu kabla ya kufikia uhuru peak

 vijana wakifanya maombi ya kumshukuru MUNGU kwa kufika eneo la juu kabisa la mlima kilimanjaro UHURU PEAK
                     KIFUNIKA eneo linalofanyiwa maombi kwa kiimani na kufanyika matambiko mbalimbali

0 comments:

Post a Comment

 

Bongo Blogs - Blog ya Taifa

COPYRIGHT © Egy business solution DESIGN BY NANG JET 0764504595,0672804085