.

.

MUNA TOYS & STATIONERY

MUNA TOYS & STATIONERY

Monday, May 19, 2014

UMESHINDWA MARA NGAPI MPAKA HUTAKI KUENDELEA TENA?



UMESHINDWA MARA NGAPI MPAKA HUTAKI KUENDELEA TENA? Ni swali kubwa na gumu ambalo kwa siku ya leo tumependa kukuuliza wewe ambaye unafuatilia  blog yetu “JE UMESHINDWA MARA NGAPI MPAKA HUTAKI KUENDELEA TENA?
Wengi ya binadamu leo duniani wamekuwa wakikata tamaa katika vitu ambavyo wao wenyewe mioyoni mwao wanaamini kuwa ndiyo ndoto zao na mafanikio yao yalipo lakini kutokana na vikwazo wanavyokutana navyo njiani vimekuwa vikiwarudisha nyuma na kuacha kuamini tena ndoto na malengo yao hasa waliyoyapanga 




JE UMESHINDWA MARA NGAPI?
  Na wengi wetu wamekuwa wakishindwa mara moja, mara mbili au hata mara kumi na kurudi nyuma na kusahau kabisa ndoto zao na malengo yao ,na hii imechangia sana dunia ya leo kuwa na watu wengi ambao  wanafanya vitu ambavyo kiukweli sio msukumo wao wa moyoni , na kikubwa tena unakuta wameshindwa kwenye hatua ya mwanzo kabisa katika maisha yaani katika “plan A”.  hebu leo yazingatie haya maneno, unataakiwa kuzingatia sana maneno haya kama unataka kufanikiwa katika mipango na ndoto zako                

Kwahiyo unayosababu sana kwako kujishangaa jinsi ulivyokata tamaa kwenye hatua ya mwanzo tuu, wakati hata hatua ya pili ujaijaribu, ndiyo maana tunakuuliza” umeshindwa mara ngapi hata hutaki kuendelea tena?”
Hebu yatazame maneno kwa uchache ambayo  MICHAEL  JORDAN mwanamichezo maarufu dunia na mwanzilishi wa wa staili mbalimbal iza uchezaji wa basketball  nchini marekani alivyokuwa akisisitiza suala la kutokata tamaa


 Watu  wengi waliofanikiwa katika maisha ni watu walioshindwa na kushindwa lakini walipambana na ndoto zao hatimaye wakafanikiwa , ndiyo maana hatutokubaliana sana na sababu zako za kusema huwezi kuendelea tena mbele, kwani umeshindwa mara nyingi  je inatosha kushindwa kwako huko ndiyo usiendelee tena mbele
Mwisho tunapenda kukuacha na maneno haya yaende kukujenga na usijipe sababu tena ya wewe kutokuendelea mbele, maadamu mambo kwako hayajakaa sawa ujue sio mwisho endelea kupambana mpaka upate. MAFANIKIO MEMA KWAKO KWA KUENDELEA KUSOMA BLOG YETU


                                                 

0 comments:

Post a Comment

 

Bongo Blogs - Blog ya Taifa

COPYRIGHT © Egy business solution DESIGN BY NANG JET 0764504595,0672804085