Bwana mmoja alikuwa anaitwa
KAKABRAZA, alikuwa amefungwa kwenye mahabusu chafu sana,akiwa humo ndani
alimwona mdudu mdogo sana ambaye husukuma mzigo wake kwa miguu, akatulia kidogo
kumwangalia akijaribu kupandisha mzigo mkubwa kuliko yeye kwenye ukuta mrefu! Akavutiwa
kidogo na tukio hilo, akitaka kujua nini hasa ilikuwa lengo la mdudu huyo na
kama kweli angeweza kupandisha mzigo mkubwa kiasi hicho katika ukuta mrefu .
Ukuta ulikuwa kama wa mita sita hivi, basi akamshuhudia mdudu kwa mara ya kwanza akisukuma mzigo wake kwa miguu sentimita kama mia moja hivi akaporomoka nao moja kwa moja hadi chini! Tofauti na alivyofikiria KAKABRAZA kuwa kwa jinsi alivyoporomoka mdudu huyo asingethubutu tena kujaribu kupandisha mzigo unao mzidi uwezo katika ukuta huo, alishangaa kumwona mdudu anaanza tena safari ya kupandisha mzigo ule ule, safari hii alikwenda kama sentimita mia mbili na hamsini hivi, akaporomoka tena mpaka chini! Akamuhurumia na kuamini kuwa huo ndio ulikuwa ndio mwisho wake
Haukupita muda mrefu,akashangaa
kumwona mdudu anaukamata tena mzigo wake kwa miguu na kuanza kuusukuma taratibu,
safari hii alikwenda kama sentimita mia nne
kabla ya kuporomoka tena hadi chini! KAKABRAZA
akashika kichwa kwa masikitiko makubwa sana akimwonea huruma, tayari
suala hilo lilishamwingia sana moyoni KAKABRAZA na kuteka hisia zake. Akiendelea
kutafakari nini kingefuata, alimwona mdudu anaukamata tena mzigo wake
kuanza safari ya kupandisha ukuta, safari hii akavuka
sentimita mia nne na kukaribia hadi sentimita mia saba na kuporomoka tena
chini,
Kila alipoporomoka mdudu huyo alikwenda moja kwa moja hadi chini na kuanza
upya lakini safari hii alizidi alipokomea mwanzo, bila shaka kuna kitu
alijifunza na kurekebisha ndiyo maana akaenda sentimita nyingi zaidi juu! Alifanya hivyo kwa kutokukata tamaa hatimaye
akafanikiwa kumaliza mita zote sita na kupotelea darini, KAKA BRAZA alishindwa
kuvumilia akanyanyuka chini alipokuwa ameketi na kushangilia kama vile goli
limefungwa akitamka maneno haya”
KAMWE MWANADAMU HUTAKIWI KUKATA TAMAA NA
NI LAZIMA UJIWEKEE LENGO KUBWA MAISHANI MWAKO”
Kama mdudu anaweza kufanya hivi
inakuwaje mwanadamu ashindwe? Mdudu alikuwa na lengo la kuvuka ukuta, akaanguka
mara kadhaa lakini hakukata tamaa, alijifunza kutokana na makosa ya nyuma na
kuendelea na safari yake hatimaye akafanikiwa!
Hivi ndivyo wanadamu tunavyotakiwa
kufanya katika maisha yetu ya kila siku, lazima tujiwekee malengo, haiwezekani
hata kidogo kuishi bila ya malengo na kutokuelewa unataka nini, lini na
kwanini?
Neva givu ap
ReplyDeleteasante nimeona mambo yenu vijana kazi yenu ninjema
ReplyDeleteahsante sana kwako kiongozi
Delete