.

.

MUNA TOYS & STATIONERY

MUNA TOYS & STATIONERY

Tuesday, March 17, 2015

VITU MUHIMU KWAKO UNAVYOPASA KUVIFAHAMU AMBAVYO WALIOFANIKIWA WENGI DUNIANI WAKO NAVYO




Watu wengi waliofanikiwa duniani na ambao hawajafanikiwa dunia huwa tunatofautiana sana kwa vitu vidogo na hakuna suala la uchawi wala kurogana katika kufikia mafanikio yaliyo ya ukweli. Namna ambavyo namna yetu ya kuishi ilivyo na nidhamu basi ndiyo vinatufanya tutaofautiane wengine wawe matajiri na wengine masikini
Nayasema haya huku nikihusianisha maisha aliyokuwa na tajiri wa kwanza duniani ndugu BILL GATES hivi sasa na hapo awali, hii inaonesha ukiamua kucheza mchezo vizuri wa kutafuta mafanikio ya kweli hapo haina upinzania lazima ufanikiwe tuu, tunaona kuwa BILL GATES ni mtu aliyeshindwa sana darasani na katika maisha na siajabu hata kuzadharauliwa, lakini alipoamua kubadirisha maisha yake na hatimaye akawa namna alivyo sasa
Mtu mwingine ambaye naye anaonesha namna ambavyo ukiamua kubadirisha mfumo wa maisha  uwezavyo ni ERICK SHIGONGO. Shigongo ambaye historia yake inaonesha kuwa alipitia vipindi vigumu vy a kudharauliwa na kusemwa vibaya kutokana na ufukara alio kuwa nao lakini hivi leo ni miongoni mwa vijana wanaosikilizwa sana Tanzania na tajiri,kikubwa aliamua kubadilisha historia ya maisha yako, sasa hivi hapa chini ni
VITU VINNE KWAKO MUHIMU KUFIKIA MAFANIKIO YAKO YA KWELI

PAMBANA KUBADILI MATOKEO: unapoelekea kufikia mafanikio yako kuna kitu ambacho unakiona mbele yako ambacho unaamini ukifanikiwa kukibadili basi mafanikio yako yanatokea sasa ushauri ambao ninaweza kukupatia ni wewe kupambana kuyabadili matokeo mabaya yanayokuzunguka na kuweka mtazamo mwingine mpya
IJUE THAMANI YA MUDA WAKO: watu waliofanikiwa na mara nyingi huwa wanajiuliza kipi cha thamani nianchotumia muda huu , jaribu kuupa muda thamani yake usiuache upotee bure mbele yako na kuiacha siku ipite bila ya wewe kufanya jambo lenye maana
WEKA VIPAUMBELE: duniani na tunavyotembea njiani tunakutana na vitu vingi sana na siajabu kila kitu tunatamani kuvifanya lakini jambo la muhimu ambalo unapaswa kulifahamu yote hayo uwezi kufanya kwa wakati mmoja bila ya kuweka vipaumbele vyako, kwahiyo jaribu kuwa na vipaumbele vyako katika maisha
FANYA KILA JAMBO KWA UFANISI: onesha ubora wako  katika kila jambo ambalo unalifanya hii itakuwezesha wewe kuwa bora zaidi na wakipekee na utajikuta unaelekea katika mafanikio yako, haijarishi hilo jambo ni lako ama la watu Fulani ili mradi tuu umepewa nafasi ya kulifanya wewe litekeleze kwa bidii yako yote utafikia mafanikio yako
AHSANTE KWA KUENDELEA KUJIFUNZA PAMOJA NASI, WEWE NI BORA NA UNAUWEZO WA KUBADILISHA DUNIA

0 comments:

Post a Comment

 

Bongo Blogs - Blog ya Taifa

COPYRIGHT © Egy business solution DESIGN BY NANG JET 0764504595,0672804085