.

.

MUNA TOYS & STATIONERY

MUNA TOYS & STATIONERY

Friday, August 1, 2014

UKIFANIKIWA KUJITIBU HUU UGONJWA VITU VINGI UTAFANIKIWA KIMAISHA





Kitendo cha kuhairisha jambo na kulipa muda wa siku nyingine au wakati unao uwezo wa kufanya kwa wakati uliopo, limekuwa tatizo kubwa kwa wengi na limesababisha kutokuweza kufika ndoto  za wengi hususani vijana wengi huu ugonjwa ndiyo tunaouita PROCASTINATION

Sababu kubwa zinazofanya wengi wetu kuhailisha mambo na kutokufanya kwa wakati na kujikuta wanangukia katika ugonjwa huu ni pamoja na
·        UOGA WA KUANZA
Wengi na karibia kila binadamu hapa duniani anayo ndoto ya kufikia mahali fulani ila kitu kikubwa ambacho kimekuwa kikikwamisha ni UOGA WA KUANZA na kujikuta kila siku anasogeza jambo husika mbele, na kutokulifanya kwa wakati sahihi.

·        KUSIKILIZA SANA WENGINE,TOFAUTI YA UNAVYOJISIKILIZA
Hili pia limekuwa tatizo kubwa kwa wengi na hasa vijana kusikiliza sana wengine mpaka wakuambie ndiyo unaanza kufanya ,na limekuwa likikukwamisha wewe kuanza kufanya jambo unaloliamini,na unasogeza kila siku na siku zina zidi kwenda mbele

·        WENGI KUTOKUJUA NGUVU NA THAMANI YA MALENGO YAO
Binadamu tunayo malengo na kila siku huwa mipango na malengo haiishi , na  ni kwanini kile ambacho tunacho au tumekipanga hakitimii, kubwa ni hatujui nini thamani ya nini kile tunachokiwekea malengo na nguvu yake pale tutakapoamua kukifanya

·        KUJIONA KUWA NI WADOGO
Kutokana na mazingira ambayo yamekuwa yakituzunguka na jinsi tulivyozoezwa na jamii , wengi hatuanzishi  ndoto zetu kwa kuwa tumekuwa tukijiona kuwa ni wadogo kiumri na kuwa hatuwezi kufanya mambo makubwa duniani, hivyo kujikuta tunahairisha mambo mengi.

·        KUJIONA KUWA HUNA ELIMU YA KUTOSHA
Na hii ndiyo tatizo zaidi mtu kujidharau mwenyewe na kujiona kuwa hana kabisa elimu na hofu kubwa kutokana na elimu ya darasani alipoishia anajiona hawezi kuanzisha kitu chochote kipya ambacho kitaigusa jamii, na hata ambacho hakijawahi kuwepo. Kuwaza kuwa wanaostahili ni wenye degree, au diploma au wanaojua kingereza tuu

·         KUTOKUPATA MSAADA
Ni hatari Kwa kila mara kujiandaa kupokea msaada Kwa watu wengine, Na hivyo msaada usipotokea unashindwa kuendelea kufanya kitu chako na kujitegemea mwenyewe hivyo kujikuta unahairisha kila jambo ambalo unapenda kulifanya katika maisha. Ikiwa umejisikiliza ndani yako basi usihofu kuanza kwa kisingizio cha kukosa msaada

·        KUPENDA KUJILAUMU NA KUTAFUTA MTU WA KUMLAUMU
Wengi wetu na hususani watanzania vijana tunapenda kujilaumu na kutafuta mtu wa kumlaumu pale mambo yanapokuwa magumu na hivyo kushindwa kuanzisha jambo jipya katika maisha, na kujikuta kila siku unatafuta mtu wa kumlaumu, kusogeza jambo




2 comments:

  1. RESPECT TO YOU AND ASANTE KWA KUNIONGEZA UMENIFANYA NIZIDI KUAMINI KWAMBA HAPA NILIPO NI SAHIHI SAANA ASANTE NA UBARIKIWE SANA...

    ReplyDelete
    Replies
    1. NASHUKURU SANA NDUGU YANGU, NAAMINI KWA PAMOJA TUTAYAFIKIA MAFANIKIO YETU, ZIDI KUISOMA BLOG YETU

      Delete

 

Bongo Blogs - Blog ya Taifa

COPYRIGHT © Egy business solution DESIGN BY NANG JET 0764504595,0672804085