” SIO WOTE AMBAO TUNAWEZA
KUFANYA MAMBO MAKUBWA, BALI TUNAWEZA KUFANYA MAMBO MADOGO SANA KWA UPENDO
MKUBWA”
huku tukiongozwa na kauli
mbiu inayosema MIMI NITAKULINDA DAIMA vijana mbalimbali wajiji la mbeya na
waliopo nje tuliweza kuchangisha kiasi cha Tsh LAKI MOJA NA ELFU TANO MIA
TANO(105,500) kwalengo lakifariji familia ya mtoto Cosmas aliyekatwa mkono.
Ziara hii iliandaliwa na
taasisi ya MBEYA YOUTH'S pamoja na YWCA MBEYA ambapo ili husisha watu
mbalimbali waliopo ndani ya jiji la Mbeya na nje.
dhamira yetu kuu ilikuwa ni
kumfariji mtoto na mama yake ambao kwa sasa wanaishi kwa hofu sana sana. Mtoto
COSMAS (umri miaka 6) alikatwa na kuondolewa kiganja chake cha mkono na watu
wasiojulikana huko maeneo ya RUKWA ,kwa sasa yupo katika hospitali ya RUFAA
MBEYA akiendelea na matibabu vizuri.
Familia hii bado ina uhitaji
mkubwa sana wa kifedha na ulinzi ili maisha yao yawe salama sana.
MTOTO COSMAS ni zaidi ya
unavyomuona katika picha, kiukweli anateseka sanaa, WANAHITAJI MCHANGO WAKO WA
HALI NA MALI SANA,
Tunatoa shukrani kwa redio za
SWEET FM , na ROCK FM kwa moyo wa kujali na kutuwezesha kusikika maeneo
mbalimbali juu ya kilio cha vijana wa jiji la Mbeya na watanzania kwa ujumla
kuhusiana na utesaji wa mtoto baraka
UKISUKUMWA KILA MARA NENDA
KAMFARIJI MTOTO COSMAS BARARA
ELLY BONKE(aliye mbeba mtoto cosmas) Mama wa mtoto, pamoja na ROBERT ELIAH
Safari ya kuelekea ndani ya hospital ya rufaa katika WODI no 8, alimolazwa
Tukitafakari juu ya tukio la mtoto kukatwa mkono
Shadrack na Herman vijana wa jiji la Mbeya miongoni wa waliojitokezaa kumfariji
EDDY CHONGOLO (mtangazaji wa ROCK FM) akifanya mahojiano na baadhi ya vijana
JULIUS JAIRO na DEBORA NJULUMI wakikabidhi msaada wa TSH 105,500 kwa mama wa COSMAS
Sefania Kajange na Robert Eliah wakiwa na watoto tulioenda kuwaonaa
Shah Mjanja akiwa pamoja na mtoto COSMAS BARAKA aliyekatwa mkono
mama wa mtoto akisimulia namna ilivyokuwa na walivyovamiwa
Mtoto baraka mwenye umri wa miaka 6 aliyekatwa mkono
TUNAWASHUKURU NYOTE MULIOWEZA KUCHANGIA KWA AJILI YA MTOTO COSMAS, TUZIDI KWENDA TENA NA TENA
UKITAKA KUWASILIANA NASI 0764761900









0 comments:
Post a Comment