Jambo linaloweza kuwa la busara sana
kwako ni wewe kutazama ndani yako unaona nini ambacho si rahisi kwa mtu
mwingine kujua malengo na nia iliyomo ndani yako. Inakuwa ngumu kwa mtu aliyeko nje kujua wewe unataka kufika wapi
na una malengo yapi?.
Watakuja hata uliokuwa unawaamini
kuwa watakusaidia katika mambo mbalimbali watakupinga na tena sio kukupinga kwa kikwango
kidogo, ni sana na watalenga kukunyamazisha hata uwezo uliokuwa ndani yako
usionekane tena.
lililo jema sana kwako wewe ni
kutokusikiliza namna ya wengine wanakatishaje tamaa na wanasimuliaje namna usivyoweza kufanikiwa katika jambo unalotaka
kulianzisha.
Asilimia kubwa ya watu waliofanikiwa
duniani leo hii walipingwa sana lakini ubishi na uking’ang’anizi wa ndoto na
jambo waliloliamini ndiyo uliowafikisha mahali walipo na hatimaye wakafanikiwa sana.
USIOGOPE, UNAVYOPINGWA NA WALA WAPINGAJI NA
WAKATISHAJI TAMAA HAWATAISHA DUNIANI KAMWE, TAZAMA UNAONA NINI NDANI YAKO? NA TENDA KWA BIDII





0 comments:
Post a Comment